Thursday 30 May 2013

Wenye divisheni ziro 30,000 wafaulu Matokeo ya Kidato cha Nne, 2012

Wanafunzi 30,063 waliopata daraja sifuri katika matokeo yaliyopita, wameula baada ya kupandishwa hadi daraja la nne kutokana na ukokotoaji upya wa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne yaliyofanywa na Baraza la Mitihani la Taifa (Nacte) na kutangazwa jana.
Marekebisho hayo yalifanyika baada ya kufutwa kwa matokeo ya awali yaliyotangazwa Februari 18, mwaka huu.
Kufutwa kwa matokeo hayo, ilikuwa ni utekelezaji wa sehemu ya mapendekezo ya Tume iliyoundwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, baada ya wanafunzi 240,909 kupata daraja sifuri kwenye matokeo yaliyotangazwa mara ya kwanza.
Akitangaza matokeo hayo jana, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa alisema sasa watakaokuwa na sifuri ni 210,846 sawa na asilimia 56.92 wakati wavulana wakiwa ni 104,259 na wasichana 106,587.
Hiyo ina maana kuwa sasa ufaulu umepanda na kuwa asilimia 43.08 badala ya ule wa kwanza ambao ulikuwa asilimia 34.5.
Dk Kawambwa alisema kutokana na ukokotoaji mpya wa matokeo ya sasa, idadi ya wanafunzi waliofaulu mtihani huo kwa daraja la kwanza mpaka la nne imeongezeka na kufikia wanafunzi 159,747 kutoka 126,847.
Wanafunzi waliopata daraja la kwanza ni 3,242 wavulana wakiwa ni 2,179 na wasichana 1,063 ikiwa ni asilimia 0.88 ya matokeo yote, daraja la pili ni 10,355 sawa na asilimia 2.8 wavulana wakiwa 7,267 na wasichana 3,088.
Waliopata daraja la tatu ni 21,752 sawa na asilimia 5.87 wavulana wakiwa 14,979 na wasichana 6,773, daraja la nne ni 124,260 sawa na asilimia 33.54 . (www.mwananchi.co.tz)
Tembelea www.necta.go.tz

No comments:

Post a Comment